Psalms 150

Msifuni Bwana Kwa Ukuu Wake


1 aMsifuni Bwana.

Msifuni Mungu katika patakatifu pake,
msifuni katika mbingu zake kuu.

2 bMsifuni kwa matendo yake makuu,
msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.

3 cMsifuni kwa mvumo wa tarumbeta,
msifuni kwa kinubi na zeze,

4 dmsifuni kwa matari na kucheza,
msifuni kwa kinanda cha nyuzi na filimbi,

5 emsifuni kwa matoazi yaliayo,
msifuni kwa matoazi yavumayo sana.


6 fKila chenye pumzi na kimsifu Bwana.

Msifuni Bwana!
Copyright information for SwhKC